Posts

ITAMBUE SONONA(DEPRESSION)

Image
Sonona(Depression) ni mojawapo ya magonjwa ya akili ambayo madhara yake katika mustakabali wa maisha ya mtu binafsi pamoja na watu wanaomzunguka sio mazuri sana,madhara haya huweza kuleta hali ya sintofahamu kwa watu wanaomzunguka mtu aliye katika hali hiyo wakati mtu mwenyewe aliye katika hali ile hujiona kawaida kwa kuwa ndio hali inayomfanya ajisikie ahueni. Sonona(Depression ) ni hisia za huzuni na masononeko azipatazo mtu kutokana na matokeo ya mifumo mbalimbali ya maisha kama vile mahusiano,shule,kazi na mambo mengine yanayochukua nafasi ya muhimu katika maisha ya mtu binafsi. Hisia hizi ambazo mara nyingi huwa katika mfumo hasi,hutokana na matokeo yasiyotarajiwa na mtu katika jambo fulani ambalo anaweza kuwa alilipa nafasi kubwa sana katika maisha yake,lakini jambo hilo likatokea kuwa tofauti na kuingilia au kuvuruga kwa kiasi kikubwa mfumo wa kufikiria na kutenda wa mtu. Zitambue dalili za mtu mwenye Sonona(Depression) Kujisikia huzuni na maumivu ndani ya nafsi(Dep

The Dillema of the Only Child(Tabia za watoto wa Pekee)

Image
Because only children do not have siblings with whom to interact, they learn to be children on their own. Parents and peer groups can help, but ultimately children become conditioned to depend on themselves. Says one adult with only child, "Possibly the best part was developing the ability to enjoy being alone and to entertain myself. I have always had plenty of friends, yet people are surprised by how much of a loner I can be". Although this self-sufficiency can have its benefits, it can also mean that only children are inherently alone as their personalities develop.Because only children must develop in social situations that may not be suited to their personalities, the concepts of introversion and extraversion must be re-evaluated in the consideration of only children. Ultimately, an only child's environment forces him or her to take on both characteristics of introversion and extraversion despite natural inclinations to be one or the other. A naturally int

CHANZO CHA UKOROFI NA UTUNDU

Image
Familia nyingi sana hasa wazazi mara nyingi hulalamika sana juu ya baadhi ya tabia za watoto wao ambazo huonekana ni chanzo cha migogoro ama katika familia ama katika jamii inayoizunguka familia hiyo. Tabia hizi huonekana kuwa si kero tu bali ni usumbufu wa hali ya juu sana,kwani huwafanya wazazi kupoteza muda kwa kiasi kikubwa katika kuhakikisha hali inakuwa shwari.   Kutokana na kutokuwepo kwa hali ya ukaribu zaidi kati ya wazazi na watoto,hali hii imekuwa ni ngumu sana kwani baadhi ya wazazi wamekosa na hawana njia sahihi ya kukabiliana na hali hii. Lakini ukweli ni kwamba hali hii inayowakumba watoto wengi ni matokeo ya kisaikolojia,ambapo mtoto anapokuwa mdogo zaidi kutokana na hatua mbalimbali za ukuaji anazopitia,ama kuna hatua fulani hakuipita vizur ama hakuipitia kabisa. Na mwisho wake amejikuta akikosa changamoto za muhimi ambazo huweza kumfanya kujifunza baadhi ya vitu ambavyo ni muhimu sana. Ukosekanaji ama upungufu wa ukaribu kati ya mtoto na mzazi huweza kumsab

JE WAJUA UTAJIRI UNAOMILIKI KATIKA MAISHA YAKO

Najua nimesema utajiri wengi watakua wameshtuka na kusubiri kwa hamu kuona ni utajiri gani huo.Kwa ujumla hakuna mtu asiyependa kuwa tajiri na maisha yetu kwa ujumla yametawaliwa na hamu ya kuwa matajiri kwa kuwa na umiliki wa mali nyingi sana ambazo zinaweza kumsaidia mtu kufanya kile anachokitaka kwa wakati anao utaka,ili afikie kile anachokitaka bila usumbufu wowote. Mtu yeyote aliye na umiliki wa mali nyingi na za kutosha hupenda kujiita ama kuitwa tajiri,lakini mali hizo anazomiliki anashindwa kutambua kuwa ni vitu vinavyoweza kuisha thamani muda wowote ule(material things).Na utajiri huo ambao huyo mtu anao hutegemea kwa kiasi kikubwa utajiri wa kipekee ambao wenyewe hauhitaji nguvu ya ziada katika kuulinda isipokuwa umakini tu katika kuutumia. Leo nataka utambue kuwa kila mtu ni tajiri,tena tajiri wa kutupwa,kila binadamu anamiliki rasilimali(resources) nyingi sana katika kichwa chake. Rasilimali hizi humzalishia faida nyingi sana ambazo huonekana na zingine zisizoonekana.

JE,WAJUA KUWA UNA TATIZO LA KISAIKOLOJIA?

Image
Katika maisha yako ya kila siku kuna mambo mengi sana unapenda kuyafanya na pia kuona watu wengine wakiyafanya,katika hali ya kawaida ni vigumu sana kuweza kutambua kwa haraka kuwa kitu au jambo unalolifanya si la kawaida kwa sababu tu umezoea kulifanya.Katika maisha ya sasa tunayoishi na jinsi hali halisi ya maisha inavyoonekana hasa kwa nchi yetu ya Tanzania,watu wengi sana hujikuta wakifanya na wakiishi maisha ambayo hayana uhusiano halisi na jinsi mtu anavyotakiwa kuishi. Changamoto mbalimbali za maisha pamoja na ukosefu/upungufu wa mahitaji ya msingi,ni vitu ambavyo huchangia kwa namna moja au nyingine kuwafanya watu waishi na kufanya mambo yasiyo ya kawaida na mwisho wa siku hali hii inapoendelea kumkuta huyu mtu huishia kupata matatizo ya kisaikolojia. Matatizo ya kisaikolojia ni tabia ambazo mtu huonekana kuwa nazo zikiwa zinaambatana na dalili mbalimbali za kisaikolojia.Tabia hizi kwa kiasi kikubwa huathiri maisha ya mtu ambaye huonekana kuwa nazo.Baadhi ya tabia hizo ni

NINI CHANZO CHA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO?

Image
Katika maisha ya kila siku ya viumbe hai,hali ya ukaribu huonekana zaidi mara kwa mara. Ukaribu huu huweza kusababishwa na mazingira waliyomo,vitu wanavyofanya na mambo wanayopenda kwa pamoja.Lakini kwa binadanu hali ya ukari husababishwa na malengo maalumu kati ya mtu na mtu,ukaribu huo huweza kusababishwa na vitu tofauti tofauti vinavyoendana kati ya mtu na mtu kama vile malengo,mitazamo,upendo,uhitaji,hisia na mambo mengine mengi yanayoweza kuwa sehemu kubwa ya kuwaleta watu karibu. Mahusiano haya au ukaribu huu unaweza kuwa wa aina tofauti kutegemeana na dhamira iliypo kati ya watu wawili,na ndipo hapo tunapata mahusiano ya kifamilia,ya kimapenzi,ya kikazi,ya kijamii,ya kirafiki na aina nyingine zote kutegemeana na dhamira pamoja na malengo yenu. Migogoro ni kitu ambacho huweza kwa kiasi kikubwa sana kudumisha ama kuzorotesha na hata kuharibu kabisa mahusiano kati ya mtu,na si watu au binadamu pekee lakini pia hata wanyama na viumbe wengine pia hukumbana na changamoto ambazo h

NI NINI CHANZO CHA HASIRA

Image
Acid ni kemikali ambayo ni hatari sana,kemikali hii inapowekuwa katika chombo huathir zaidi chombo hicho kuliko vitu vingine vyote vilivyopo jirani na chombo hicho. Vivyo hivyo ndivyo mtu anapokuwa na hasira,kwani hasira ni hali ambayo humuathiri zaidi aliyenayo kuliko mtu mwingine zaidi,kwani maumivu ya hasira huyapata yle aliyenayo zaidi kuliko aliyechanzo cha hasira hiyo. Kila kiumbe aliye hai hupatwa na hasira,yaani wanyama,ndege na hata wadudu wote hupatwa na hasira.Hivyo hasira ni hali isiyoepukika katika hali ya kawaida. Mwanasaikolojia T.W Smith  yeye alisema kuwa, hasira ni muhemko usio epukika,muhemko huu unaotokana na hisia hasi juu kitu,jambo au hali fulani.Nuhemkohuu hutofatiana kutoka katika hali ya kawaida hadi katika hali inaweza kusababisha madhara kwa mtu binafsi na hata kwa watu wengine. Binadamu ndiye kiumbe amabaye hupatwa na hasira mara kwa mara kuiko viumbe wengine wote,na hasira hii huchukua muda mrefu hadi kuisha,na hii hutegemeana na uwezowa mtu